Poems

Uniimbie

Uniimbie  
Si wimbo 
Si shairi
Si utenzi
 
Uniimbie 
Hisia zako na zangu 
Hisia za wanaAdamu
Hisia za wavuja
jasho na damu
 
Uniimbie 
Ya maisha bora
Yenye ustawi na Utu
Yenye mwanga bila luku
 
Langu Dua
Likiwaka jua 
Ukiiandama mwezi
Giza litakimbia
Mende zitaparaganyika